Wiki hii inayoisha nilibahatika kushirika Selous Marathon moja ya marathon zilizojizolea umaarufu sana hapa nchini kwa miaka ya karibuni.Safari hii nilichagua kukimbia mbio za milimani maarufu kama trail.Haikuwa rahisi hata kidogo lakini nashukuru niliweza kukamilisha mbio hizo na kupata medali yangu.
Tuachane na hilo sababu sio haswa dhumuni la makala hii fupi.Kipindi cha nyuma niliwahi kushirikisha juu ya mwanariadha wa Kitanzania John Akhwari ambaye alishiriki mashindano ya riadha nchini Mexico mwaka 1968.
Kwenye mbio zile za kilometa 42 kwa bahati mbaya sana wakati tu John anaanza alipata shida kwenye goti na mabegani.Hii ilitokana na hali ya hewa ya milimamilima iliyopo nchini Mexico.
Hilo halikuwa sababu ya John Akwar kuahirisha mbio hizo ambazo zilishuhudia idadi kubwa ya wanariadha kuishia njiani.
Waliofanikiwa kufika mwisho wa mbio walikuwa wameshapewa medali zao ila hadi giza linaanza kuingia ndipo alipoingia bwana John Akhwari.Watu waliokuwepo Uwanjani walimshangilia licha ya kuwa ndio alikuwa mtu wa mwisho kwenye mbio zile.
Kitu kikubwa ni pale mwandishi wa Habari alipomuhoji kwa nini hakuahirisha mbio zile pamoja na changamoto aliyoipata.Yeye alijibu ‘Nchi yangu haikunituma maili elfu tano Kuja hapa kuanza tu mbio,ilinituma maili elfu tano Kuja kumaliza mbio’.
Unaweza kuipata video kupitia YouTube.
Somo kubwa ambalo tunaweza kuondoka nalo hapo ni UVUMILIVU.Baada ya kujua nini haswa tunataka kwenye maisha yetu uvumilivu unahitajika sana.Sio kwenye fedha,biashara, kazi,mahusiano au maisha kiujumla uvumilivu unahitajika sana.
Kama kuna kitu kingine muhimu cha kuwafundisha watoto wetu basi ni UVUMILIVU.
Makala hii imeandikwa na Innocent Didas.
Mzazi,mtaalam wa malezi na mjasiriamali.
0764639570
Morogoro Tanzania.